Wakati matokeo ya kura zilizopigwa katika uchaguzi mkuu wa Tanzania bara na visiwani yakiendelea kutangazwa, baadhi ya wananchi visiwani humo wametoa maoni yao juu ya mwenendo wa uchaguzi huku mgombea urais visiwani humo kwa tiketi ya chama cha ACT Wazalendo, Maalim Seif akiitisha maandamano baada ya kutokuridhishwa na mwenendo wa uchaguzi huo. Hata hivyo Maalim alikamatwa na polisi baada ya wito huo. #Kurunzi 29.10.2020